Saturday 15 November 2014

"MTOTO WA MIAKA 5 AFAULU MTIHANI WA MICROSOFT"


Mtoto huyo anaetokea Coventry amekua ndiye mtu mwenye umri mdogo sana kuwa na ujuzi wa maswala ya Computer duniani.Mtoto huyo anaekwenda kwa jina la Ayan Qureshi sasa ni Microsoft Certified Proffessional (MCP) baada ya kufaulu mtihani wa kiufundi unaotungwa na na kuratibiwa na Microsoft akiwa na umri wa miaka mitano (5) tu.

        Ayan ambae kwa sasa ana miaka 6,baba yake ni mtaalamu na mshauri kwenye maswala ya teknolojia,ametengeneza mtandao wa komputa nyumbani.





Wednesday 29 October 2014

"KUTANA NA KIJANA ANAYETENGENEZA MAMILIONI YA PESA KWA KUSAFISHA VIATU"






















Haijalishi ni aina gani ya viatu gani unavaa katika mkutano muhimu wa biashara swala kubwa la msingi ni viwe vinang'aa na vyenye mvuto.Picha juu hapo inaonesha kijana aliyekuwa maarufu kwa uuzaji wa Mayai akifanya kazi yake ya 'Shoe Shiner'.Kijana huyo anaekwenda kwa jina la Lere Mgayiya anasema wana kampuni kubwa ya kusafisha viatu kwa Afrika nzima,"Wakiwa ndani ya Johansburg wanasafisha pea 350 kwa siku ,Pea 120 Capetown,na 120 zingine kutoka Durban.Kampuni yake imeajiri wafanyakazi 45 ambao kwa sasa wametawanyika kwenye Viwanja vya ndege vitatu.Hadi sasa ana utajiri wa Randi Milioni 2.5 sawa na Dola 227,000 kwa kazi hiyo....

Thursday 16 October 2014

"USHAWAHI KUONA MASHINDANO YA NDEVU?",ANGALIA WATU NA NDEVU ZAO NI SHEEEEDA...!!






















   Dunia ina mambo na vijambo,ukistaajabu ya Musa utayaona ya Firauni,duniani watu tumezoea kuona mashabiki wa fani mbalimbali ikiwemo Mpira wa Miguu,gofu,nk.Ila mwaka huu 25/10/2014 kutakuwa na shindano maarufu la "NDEVU NA MUSTACHI",litakalofanyika Portland,Oregon.Inatarajiwa watu 3000 ''Wenye Ndevu''  kuhudhuria shindano hilo na watashindana  katika vipengele mbalimbali....!!!



Tuesday 14 October 2014

"KAMA KUBUSU TU UNAFUKUZWA KAZI,JE UKILA RUSHWAAA ITAKUAJE''

ASKARI WAKIWA WANAPEANA MABUSU MOTO MOTO MUDA WA KAZI.

Ni muda upi ambao ni muafaka kwa wewe kumbusu rafiki au mtu wako wa karibu?,Picha hapo juu inaonesha askari wawili wakipigana busu lililopelekea wao kupoteza kazi ''KWA AJILI YA BUSU TU?''.Kwa mtazamo wa kawaida hawa askari wawili hawakufikiria kama swala lingefika hatua mbaya ya kupelekea kufukuzwa kazi.Picha hiyo iliyopigwa Kagera-Kaskazini Magharibi mwa Tanzania-Ikionesha wawili hao wakipeana busu huku wakiwa wamevalia unifomu za kazini na hicho tu kilichukuliwa kama kigezo cha kuwafukuza kazi.

Picha hiyo iliyopakiwa kwenye intanenti na askari wa tatu,ambaye ndiye aliyepiga picha hiyo,iliyoibua mamlaka husika kulivalia njuga swala hilo,ndani ya Mamlaka ya Polisi mjini Kagera.Henry Mwaibambe ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa akiongea na BBC kuhusu hatua zilizochukuliwa,na kutetea maamuzi ya idara.Ingawa kwenye mitandao mingi ya kijamii watu wengi wamekua na maoni tofauti" niliwahi kuona picha ya aliyekua Raisi wa Marekani Reagan akimbusu mke wake,na hakuna aliyetaka kumwajibisha'',Mwingine akaongezea kwa kusema "Akari wawili wanapobusiana adhabu yao ni kubwa kuliko wala rushwa"
















Sunday 12 October 2014

"KIMBUNGA HUD HUD CHALETA MAAFA NCHINI INDIA''

  Kimbunga cha Hud Hud kinaendelea kimeuvuruga ukanda wa mashariki wa India,na kusababisha uharibifu uliopelekea kuwaondoa watu 350,000 kama hatua za usalama kwa raia hao.

   Hata hivyo inasemekana watu watatu wamekufa katika mji Andhra Pradesh na watatu pia katika mji wa Orissa.Kimbunga hicho kilichowekwa kwenye kundi ''Madhara sana'' kimeleta upepo uliokuwa unasafiri kwa mwendo kasi wa kilometa 205 kwa saa (205Km/h),kilivyokua kinapita pwani ya karibu na jiji la Visakhapatnam.Upepo huo mkali na mvua zimesababisha uharibifu wa miti,kukatika kwa huduma ya umeme pia uharibifu wa mazao shambani na majengo katika miji yote miwili.


KWA HABARI ZAIDI>>>

Saturday 4 October 2014

"MCHUNGAJI WA AINA HII KAA NAE CHONJO"






















Hiki ni kipande cha tukio la mchungaji aliyefumaniwa hotelini na mwanadada mrembo imeleta mkanganyiko pia imepelekea sintofahamu kwa wakazi nchini Kenya.Ilirushwa katika kipindi cha taarifa ya habari ya Kenya,ilionesha mchungaji wa  kanisa la Anglikana Charles Githinji akiwa amevalisha sehemu tu ya mwili wake,akiwa na msichana binti mrembo.Huku anaedaiwa kuwa na mume wa msichana mrembo akiingia na timu ya watu wa televisioni na kamera kushuhudia tukio hilo..

Friday 3 October 2014

"LIONEL MESSI KUSHTAKIWA KWA KUKWEPA KULIPA KODI"



























Nyota wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina anatarajiwa kupandishwa kizimbani kwa tuhuma ya kukwepa kodi,jaji wa Nchini Hispania ametanabaisha.Messi na baba yake Jorge wanatuhumiwa kwa kukwepa kodi inayofikia Euros milioni 4.Mtu na babae wamekataa tuhuma hizo huku wakipewa siku 5 za kukata rufaa juu ya shauri hilo.

Tuesday 30 September 2014

" EBOLA YAINGIA USA"






















Kesi ya kwanza ya Ebola imethibitishwa ndani ya ardhi ya Marekani,Dallas- Texas.Maofisa katika hospitali ya Dallas wamesema mgonjwa huyo ambae hakutajwa jina wamemtenga ili kuendelea kumhudumia kwa umakini na ukaribu wa hali ya juu.Inasemekana mgonjwa huyo alipata maambukizi hayo akiwa nchini Liberia kabla dalili hazijaanza kujitokeza.
KWA HABARI ZAIDI>>>

"TAZAMA MATOKEO YA MECHI ZA UEFA LEO,NA MSIMAMO KATIKA MAKUNDI"

Fungua hapa kupata matokeo ya mechi za uefa na msimamo wa makundi

Sunday 28 September 2014

"MESSI AFIKISHA MAGOLI 401 KWA TIMU YAKE YA BARCELONA NA ARGENTINA"




















Mshambuliaji mahiri wa Barcelona Lionel Messi,ambaye pia ni mchezaji bora wa dunia kwa  mara ya nne amefikisha magoli 401,katika mechi yao iliyoshudia Granada wakichakazwa goli 6 bila majibu.Messi alisema''hakutarajia kama angeweza kufikia mafanikio ya namna hii''.

Sunday 21 September 2014

"VAN GAAL ASHANGAZWA NA KICHAPO CHA GOLI 5 DHIDI YA LEICESTER 5-3 MAN U"






















Leicester city waliotokea nyuma wakiwa wamefungwa goli 3-1,wameibuka kidedea leo dhidi ya Manchester United.Man U walipata pigo baada ya mchezaji wao Blackett kupewa kadi nyekundu.Kwa upande wa Man u pazia la magoli lilifunguliwa na RVP dakika ya 13,Di Maria dakika ya 16,Herrera 57,Kwa upande wa wenyeji magoli yao yalifungwa na Ulloa (17 na dakika ya 83 (penati),Nugent dakika ya 62 (kwa penati).Cambiasso 64 na Vardy dak ya 79.

Saturday 20 September 2014

"REAL MADRID YAUA 8,HUKU CR7 AKIPIGA HAT-TRICK",LIVERPOOL NAYO YACHEZESHWA KWATA NA WESTHAM,WHU 3-1 LFC"
















Cristiano Rolnado leo ameifungia timu yake magoli matatu huku vigogo hao wa soka wa hispania wakishinda goli 8 ugenini dhidi ya timu ya Deportivo La Coruna ambao walijipatia ushindi wa goli 2,CR ametia nyavuni dakika ya 29,48 na 78,James Rodriguez ameifungia timu yake dakika ya 36,Gareth Balle nae akifanikiwa kufumania nyavu mara 2,katika dakika ya 66 na 74,wakati huo Chicharito akifanikiwa kufumania nyavu mara mbili katika dakika ya 88.


Nao majogoo wa London wanaendelea kuchechemea kwa kukubali kichapo cha goli 3 dhidi ya West Ham United huku Liverpool wakifanikiwa kupata goli moja kupitia kwa mchezaji Sterling.Mambo yalionekana kuwaendea kombo dakika ya kwanza tu ya mchezo.Goli la Reid na Diafro Sakho yaliwapa nguvu West ham kumiliki sehemu kubwa ya  mchezo.




Friday 19 September 2014

"KUTANA NA BABA WA WATOTO 26 'ANAEHUBIRI' KUHUSU UZAZI WA MPANGO"


























Katika nchi nyingi,ni  kawaida kwa mwanamke hasa maeneo ya vijijini kufanya kazi zaidi ya waume zao,ilhali wanaume wanapata muda mwingi wa kupumzika.Kutokana na uzoefu wa Kouayou almaarufu "Nabii".Anasema "Kwa utamaduni wetu,jinsi unavyopata watoto wengi,ndivyo unavyokua tajiri na mwenye ufahari nami nimeweka rekodi hiyo kijijini kwangu".


" WALIOKUFA KARNE 7 ZILIZOPITA WAKUTWA "WAMESHIKANA MIKONO ''






















Dunia ina mambo hata kifo kimeshindwa kuwatenganisha hawa wanaosadikiwa kufa miaka 700 iliyopita baada ya timu ya mambo ya kale kugundua uwepo wa kaburi hilo katika mji wa Leicester,walikuta wawili hao wakiwa wameshikana mikono.

Sunday 14 September 2014

"MWENYE HIV AAMURIWA NA MAHAKAMA KUACHA KUWAAMBUKIZA WATU KWA MAKUSUDI"






















Jaji wa mahakama ya Seatle nchini Marekani ameamuru kijana anaetambulika kwa jina la "AO",aache mara moja kueneza ugonjwa na kwenda kupata tiba mara  moja,baada ya kuwaambukiza watu nane (8) ndani ya miaka minne (4).Ametakiwa kwenda kuwaona wataalamu wa maswala ya Ushauri ili kuwalinda wapenzi wake wengine dhidi ya  maambukizi.


Saturday 13 September 2014

"ATLETICO MADRID WAENDELEZA UBABE KWA REAL MADRID, HUKU NEYMAR AKITUPIA 2''






















Watemi wa soka nchini Hispania wamekubali kichapo cha goli 2-1,dhidi ya wapinzani wao Atletico Madrid,wababe hao waliopata  goli kupitia kwa Cristiano Ronaldo aliefunga kwa penat Dakika ya 26,Magoli ya Atletico Madrid yamefungwa na Tiago katika dakika ya 10 huku la ushindi likifungwa na Turan katika dakika ya 76.

KWA HABARI ZAIDI>>>

NDANI YA NOU CAMP
Neymar aamsha mashabiki wake mara mbili,Neymar aliyetokea Benchi alifanikiwa kufunga magoli 
mawili,katika dakika ya 79 na 84,wakicheza na timu iliionesha ushindani mzito Athletic Bilbao





















KWA HABARI ZAIDI>>>



"COSTA ATUPIA HAT-TRICK,CHELSEA YAPAA HUKU LIVERPOOL IKIKALISHWA ANFIELD"






















Diego Costa amefanikiwa kupiga goli zake 3 ndani ya mechi moja yaani ''hat-trick'' ,magoli hayo yamefungwa katika dakika ya 45,56,na 67 huku Loic Remy akifunga pazia kwa kufunga bao la 4 dakika ya 81.Huu ni ushindi wa 4 mfululizo hiyo inaendelea kuwathibitishia   ushindi wa 100% tangu kuanza kwa ligi hiyo.Huku magoli ya Swansea yakifungwa na Terry dakika ya 11,na Shelvey 86.

KWA HABARI ZAIDI>>

NDANI YA ANFIELD MAMBO SI SHWARI

Liverpool nao wameteleza kwa kukubali kuchapwa goli moja,wakiwa ndani ya uwanja wao wa Anfield walipofungwa goli la mapema katika dakika ya 9 lililofungwa na Gabriel Agbonlahor,ambao ushindi huo umeipeleka Aston Villa kwenye nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.



Tuesday 9 September 2014

"UNYANYASAJI MAJUMBANI,UNAUA ZAIDI YA VITA YA WENYEWE KWA WENYEWE''


























Ripoti ya Umoja wa Mataifa  imeweka bayana kwamba wengi wanakufa kutokana na ukatili wa nyumbani kuliko wanavyokufa kwenye uwanja wa mapambano,inayopelekea mamilioni kupotea kutokana na vifo hivyo vinavyosababishwa na ukatili majumbani.

  Ripoti hiyo inaendelea kuweka bayana kwamba Ukatili majumbani hasa unaowalenga Wanawake na Watoto,unauwa watu wengi kuliko athari halisi zinazotokana na Vita hiyo,inayogharimu dunia Dola Trilioni 8 kwa mwaka.....!!!

    
                                KWA HABARI ZAIDI>>>




Saturday 6 September 2014

"WALIOFUNGWA KIMAKOSA KUTOKANA NA KESI YA UBAKAJI WAFIDIWA DOLA ZA KIMAREKANI MILION 41"


Jaji wa mahakama ya rufaa ya  ameamuru malipo ya Dola za kimarekani milioni arobaini na moja ($41) Kutoka Jiji la New York kulipwa kwa vijana watano waliotumikia kifungo cha miaka 30 jela  kimakosa baada ya kushtakiwa kwa kosa la ubakaji mwaka 1989.Malipo hayo ni fidia kwa wahanga au kuwafuta machozi, baada ya mwaka 2002 mtuhumiwa aliyetenda kosa hilo kukiri makosa hayo.


Friday 5 September 2014

"SHIRIKA LA AFYA DUNIANI LASHAURI KUTUMIA DAMU ZA WALIOPONA EBOLA KUTIBU EBOLA"

Damu iliyotoka kwa watu waliopona Ebola yaweza kutumika ili kutibu wagonjwa wa Ebola...!!

Ule usemi wa dawa  ya moto ni moto unaotumiwa sana na waswahili nadhani unaweza ukakubaliana na hili tamko lilitolewa na Shirika la afya duniani ya WHO limetangaza kwamba "Damu za watu waliopona kutokana na maambukizi ya Ebola inapaswa itumike kuwatibu wagonjwa wapya walioathiriwa na ugonjwa huo".

Afrika Magharibi ndiyo imepata madhara makubwa tangu ugonjwa huo uanze kuenea katika ukanda huu zaidi ya watu 2000 wameshapoteza maisha.























"GOLI KIPA ALIYEINGIA KWENYE KITABU CHA GUINESS,HUYU SI MWINGINE NI ASMIR BEGOVIC"






















Huyo si mwingine bali mlinda mlango wa timu ya Stoke City Asmir Begovic,ambaye jina lake limefanikiwa kuandikwa katika kitabu cha rekodi za dunia cha Guiness baada ya kufunga goli la mbali sana.Alifunga goli hilo kwenye mechi iliyopigwa mwezi Novemba mwaka jana kati ya Stoke City na Southampton iliyoisha kwa suluhu ya 1-1,Alifunga goli hilo akiwa umbali wa mita 91.9 toka lango la wapinzani.

                                   KWA HABARI ZAIDI>>>

"KATIKA KARNE YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA,MAJI NI ANASA NA SIO HITAJI LA MUHIMU LA BINADAMU"

Baada ya miaka 30 ya njaa iliyokithiri nchini Ethiopia,bado upatikanaji wa maji ni wa mashaka hasa ukizingatia umuhimu weneyewe wa maji kwa binadamu kama usemi maarufu usemao maarufu ''MAJI NI UHAI''.Ikiwa asilimia 52 ya watu wote inapata huduma bora za maji lakini,asilimia 10 pekee ndio waliounganishiwa bomba hadi majumbani mwao.Katika maeneo ya vijijini ni asilimia 1 tu  iliyounganishwa na huduma hii muhimu katika maisha ya binadamu..


KWA HABARI ZAIDI>>>

Hii ina maana kubwa sana.Kwa nchi ambayo uchumi wake unategemea Kilimo,upungufu wa maji hauathiri Uchumi pekee bali  unaathiri maisha ya kila siku ya wakazi hawa ambao kujikimu kwao kunategemea mavuno ya kila msimu.Mara nyingi nchi maskini kama ya Ethiopia,yenye wakazi wengi,inakumbwa sana na janga la kukosekana kwa huduma ya maji.


Kuna mambo mengi yanayochangia ukosefu wa maji safi na salama,kuanzia uharibifu wa Mazingira unaosababishwa na ukataji ovyo wa miti,majanga ya kiasili kama Mafuriko na mabadiliko ya tabia nchi....!!!


Thursday 4 September 2014

"ABIRIA KADHAA WAHOFIWA KUFA BAADA YA BASI KUSOMBWA NA MAFURIKO"


Takribani abiria 70 wanahofiwa kufa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kusombwa na mafuriko katika jimbo la Kashmir,inaripotiwa.Ajali hiyo iliyotokea Alhamisi Kusini mwa Wilaya ya Rajouri katika ukanda wa Himalaya ambapo imekumbwa na mafuriko makali tangu miaka 22.

Wednesday 3 September 2014

"HII INAUMA,JAMAA WAKUTWA HAWANA HATIA BAADA YA KUFUNGWA JELA KWA MIAKA 30"


Vipimo vya vinasaba vilionesha ndugu hao wawili,ambao wana matatizo ya akili pia walikua ni vijana wadogo chini ya umri wa miaka 20,walioingia hatiani kimakosa tangu 1983.Wawili hao waliachiwa huru baada ya kutumikia kifungo cha miaka 30 ikiwa ni sawa na Miongo mitatu,jela kwa kesi ya Ubakaji na Mauaji ya binti wa miaka 11 baada ya ushahidi kuwekwa wazi kupitia vipimo vya vinasaba.Machungu na manung'uniko yao hayatakwisha kamwe.




Sunday 31 August 2014

"REAL SOCIEDAD YAMCHARAZA REAL MADRID 4 KWA 2"


Real sociedad imewakimbiza mchachaka Real maadrid kwa kuichapa jumla ya goli 4 kwa 2,Ramos alieanza kufunga katika dakika ya 5,ikifuatiwa na goli la Bale dakika ya 11,Huku Martinez akisawazishia timu yake dakika ya 35,Zurutuza dakika ya 41 na 65 huku Vela akimalizia kufunga katika dakika ya 75
KWA HABARI ZAIDI>>>

"LIVERPOOL YAUA 3 DHIDI YA TOT"




















Brendan Rogers ameiongoza timu yake kushinda dhidi ya Tottenham,huku akifikisha mechi ya 100 tangu kuanza kuwa kocha wa Liverpool ndani ya White Hart Lane.Sterling aliyefungua pazia kwa kuifungia goli la kwanza dakika ya 8,huku Gerad akifunga kwa penat katika dakika ya 49,na Moreno alimalizia kwa kufunga goli la 3.
                          KWA HABARI ZAIDI>>>

Saturday 30 August 2014

"MAN CITY WAKALISHWA ETIHAD,MAN U WASHIKWA SHATI"




















Stoke city wamefanikiwa kuwaduwaza Man city kwa kuwachapa goli moja liliwekwa kimiani na Mame Biram Diouf mnamo dakika 58 ya mchezo,Man city walifanikiwa kuduwazwa wakicheza uwanja wao wa nyumbani.Wakati huo Man u wakikaribishwa na Burnley wamelazimishwa sare ya bila kufungana.


Friday 29 August 2014

"JIONEE TIMU YAKO IMEPANGWA KUNDI GANI,HUKU LIVERPOOL IKIPANGWA NA BINGWA MTETEZI,R MADRID"




GROUPS

GROUP A

AtléticoAtlético(ESP)
JuventusJuventus(ITA)
OlympiacosOlympiacos(GRE)
MalmöMalmö(SWE)

GROUP B

Real MadridReal Madrid(ESP)
BaselBasel(SUI)
LiverpoolLiverpool(ENG)
LudogoretsLudogorets(BUL)

GROUP C

BenficaBenfica(POR)
ZenitZenit(RUS)
LeverkusenLeverkusen(GER)
MonacoMonaco(FRA)

GROUP D

ArsenalArsenal(ENG)
DortmundDortmund(GER)
GalatasarayGalatasaray(TUR)
AnderlechtAnderlecht(BEL)

GROUP E

BayernBayern(GER)
Man. CityMan. City(ENG)
CSKA MoskvaCSKA Moskva(RUS)
RomaRoma(ITA)

GROUP F

BarcelonaBarcelona(ESP)
ParisParis(FRA)
AjaxAjax(NED)
APOELAPOEL(CYP)

GROUP G

ChelseaChelsea(ENG)
SchalkeSchalke(GER)
SportingSporting(POR)
MariborMaribor(SVN)

GROUP H

PortoPorto(POR)
Shakhtar DonetskShakhtar Donetsk(UKR)
AthleticAthletic(ESP)
BATEBATE(BLR)