Tuesday 30 September 2014

" EBOLA YAINGIA USA"






















Kesi ya kwanza ya Ebola imethibitishwa ndani ya ardhi ya Marekani,Dallas- Texas.Maofisa katika hospitali ya Dallas wamesema mgonjwa huyo ambae hakutajwa jina wamemtenga ili kuendelea kumhudumia kwa umakini na ukaribu wa hali ya juu.Inasemekana mgonjwa huyo alipata maambukizi hayo akiwa nchini Liberia kabla dalili hazijaanza kujitokeza.
KWA HABARI ZAIDI>>>

"TAZAMA MATOKEO YA MECHI ZA UEFA LEO,NA MSIMAMO KATIKA MAKUNDI"

Fungua hapa kupata matokeo ya mechi za uefa na msimamo wa makundi

Sunday 28 September 2014

"MESSI AFIKISHA MAGOLI 401 KWA TIMU YAKE YA BARCELONA NA ARGENTINA"




















Mshambuliaji mahiri wa Barcelona Lionel Messi,ambaye pia ni mchezaji bora wa dunia kwa  mara ya nne amefikisha magoli 401,katika mechi yao iliyoshudia Granada wakichakazwa goli 6 bila majibu.Messi alisema''hakutarajia kama angeweza kufikia mafanikio ya namna hii''.

Sunday 21 September 2014

"VAN GAAL ASHANGAZWA NA KICHAPO CHA GOLI 5 DHIDI YA LEICESTER 5-3 MAN U"






















Leicester city waliotokea nyuma wakiwa wamefungwa goli 3-1,wameibuka kidedea leo dhidi ya Manchester United.Man U walipata pigo baada ya mchezaji wao Blackett kupewa kadi nyekundu.Kwa upande wa Man u pazia la magoli lilifunguliwa na RVP dakika ya 13,Di Maria dakika ya 16,Herrera 57,Kwa upande wa wenyeji magoli yao yalifungwa na Ulloa (17 na dakika ya 83 (penati),Nugent dakika ya 62 (kwa penati).Cambiasso 64 na Vardy dak ya 79.

Saturday 20 September 2014

"REAL MADRID YAUA 8,HUKU CR7 AKIPIGA HAT-TRICK",LIVERPOOL NAYO YACHEZESHWA KWATA NA WESTHAM,WHU 3-1 LFC"
















Cristiano Rolnado leo ameifungia timu yake magoli matatu huku vigogo hao wa soka wa hispania wakishinda goli 8 ugenini dhidi ya timu ya Deportivo La Coruna ambao walijipatia ushindi wa goli 2,CR ametia nyavuni dakika ya 29,48 na 78,James Rodriguez ameifungia timu yake dakika ya 36,Gareth Balle nae akifanikiwa kufumania nyavu mara 2,katika dakika ya 66 na 74,wakati huo Chicharito akifanikiwa kufumania nyavu mara mbili katika dakika ya 88.


Nao majogoo wa London wanaendelea kuchechemea kwa kukubali kichapo cha goli 3 dhidi ya West Ham United huku Liverpool wakifanikiwa kupata goli moja kupitia kwa mchezaji Sterling.Mambo yalionekana kuwaendea kombo dakika ya kwanza tu ya mchezo.Goli la Reid na Diafro Sakho yaliwapa nguvu West ham kumiliki sehemu kubwa ya  mchezo.




Friday 19 September 2014

"KUTANA NA BABA WA WATOTO 26 'ANAEHUBIRI' KUHUSU UZAZI WA MPANGO"


























Katika nchi nyingi,ni  kawaida kwa mwanamke hasa maeneo ya vijijini kufanya kazi zaidi ya waume zao,ilhali wanaume wanapata muda mwingi wa kupumzika.Kutokana na uzoefu wa Kouayou almaarufu "Nabii".Anasema "Kwa utamaduni wetu,jinsi unavyopata watoto wengi,ndivyo unavyokua tajiri na mwenye ufahari nami nimeweka rekodi hiyo kijijini kwangu".


" WALIOKUFA KARNE 7 ZILIZOPITA WAKUTWA "WAMESHIKANA MIKONO ''






















Dunia ina mambo hata kifo kimeshindwa kuwatenganisha hawa wanaosadikiwa kufa miaka 700 iliyopita baada ya timu ya mambo ya kale kugundua uwepo wa kaburi hilo katika mji wa Leicester,walikuta wawili hao wakiwa wameshikana mikono.

Sunday 14 September 2014

"MWENYE HIV AAMURIWA NA MAHAKAMA KUACHA KUWAAMBUKIZA WATU KWA MAKUSUDI"






















Jaji wa mahakama ya Seatle nchini Marekani ameamuru kijana anaetambulika kwa jina la "AO",aache mara moja kueneza ugonjwa na kwenda kupata tiba mara  moja,baada ya kuwaambukiza watu nane (8) ndani ya miaka minne (4).Ametakiwa kwenda kuwaona wataalamu wa maswala ya Ushauri ili kuwalinda wapenzi wake wengine dhidi ya  maambukizi.


Saturday 13 September 2014

"ATLETICO MADRID WAENDELEZA UBABE KWA REAL MADRID, HUKU NEYMAR AKITUPIA 2''






















Watemi wa soka nchini Hispania wamekubali kichapo cha goli 2-1,dhidi ya wapinzani wao Atletico Madrid,wababe hao waliopata  goli kupitia kwa Cristiano Ronaldo aliefunga kwa penat Dakika ya 26,Magoli ya Atletico Madrid yamefungwa na Tiago katika dakika ya 10 huku la ushindi likifungwa na Turan katika dakika ya 76.

KWA HABARI ZAIDI>>>

NDANI YA NOU CAMP
Neymar aamsha mashabiki wake mara mbili,Neymar aliyetokea Benchi alifanikiwa kufunga magoli 
mawili,katika dakika ya 79 na 84,wakicheza na timu iliionesha ushindani mzito Athletic Bilbao





















KWA HABARI ZAIDI>>>



"COSTA ATUPIA HAT-TRICK,CHELSEA YAPAA HUKU LIVERPOOL IKIKALISHWA ANFIELD"






















Diego Costa amefanikiwa kupiga goli zake 3 ndani ya mechi moja yaani ''hat-trick'' ,magoli hayo yamefungwa katika dakika ya 45,56,na 67 huku Loic Remy akifunga pazia kwa kufunga bao la 4 dakika ya 81.Huu ni ushindi wa 4 mfululizo hiyo inaendelea kuwathibitishia   ushindi wa 100% tangu kuanza kwa ligi hiyo.Huku magoli ya Swansea yakifungwa na Terry dakika ya 11,na Shelvey 86.

KWA HABARI ZAIDI>>

NDANI YA ANFIELD MAMBO SI SHWARI

Liverpool nao wameteleza kwa kukubali kuchapwa goli moja,wakiwa ndani ya uwanja wao wa Anfield walipofungwa goli la mapema katika dakika ya 9 lililofungwa na Gabriel Agbonlahor,ambao ushindi huo umeipeleka Aston Villa kwenye nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.



Tuesday 9 September 2014

"UNYANYASAJI MAJUMBANI,UNAUA ZAIDI YA VITA YA WENYEWE KWA WENYEWE''


























Ripoti ya Umoja wa Mataifa  imeweka bayana kwamba wengi wanakufa kutokana na ukatili wa nyumbani kuliko wanavyokufa kwenye uwanja wa mapambano,inayopelekea mamilioni kupotea kutokana na vifo hivyo vinavyosababishwa na ukatili majumbani.

  Ripoti hiyo inaendelea kuweka bayana kwamba Ukatili majumbani hasa unaowalenga Wanawake na Watoto,unauwa watu wengi kuliko athari halisi zinazotokana na Vita hiyo,inayogharimu dunia Dola Trilioni 8 kwa mwaka.....!!!

    
                                KWA HABARI ZAIDI>>>




Saturday 6 September 2014

"WALIOFUNGWA KIMAKOSA KUTOKANA NA KESI YA UBAKAJI WAFIDIWA DOLA ZA KIMAREKANI MILION 41"


Jaji wa mahakama ya rufaa ya  ameamuru malipo ya Dola za kimarekani milioni arobaini na moja ($41) Kutoka Jiji la New York kulipwa kwa vijana watano waliotumikia kifungo cha miaka 30 jela  kimakosa baada ya kushtakiwa kwa kosa la ubakaji mwaka 1989.Malipo hayo ni fidia kwa wahanga au kuwafuta machozi, baada ya mwaka 2002 mtuhumiwa aliyetenda kosa hilo kukiri makosa hayo.


Friday 5 September 2014

"SHIRIKA LA AFYA DUNIANI LASHAURI KUTUMIA DAMU ZA WALIOPONA EBOLA KUTIBU EBOLA"

Damu iliyotoka kwa watu waliopona Ebola yaweza kutumika ili kutibu wagonjwa wa Ebola...!!

Ule usemi wa dawa  ya moto ni moto unaotumiwa sana na waswahili nadhani unaweza ukakubaliana na hili tamko lilitolewa na Shirika la afya duniani ya WHO limetangaza kwamba "Damu za watu waliopona kutokana na maambukizi ya Ebola inapaswa itumike kuwatibu wagonjwa wapya walioathiriwa na ugonjwa huo".

Afrika Magharibi ndiyo imepata madhara makubwa tangu ugonjwa huo uanze kuenea katika ukanda huu zaidi ya watu 2000 wameshapoteza maisha.























"GOLI KIPA ALIYEINGIA KWENYE KITABU CHA GUINESS,HUYU SI MWINGINE NI ASMIR BEGOVIC"






















Huyo si mwingine bali mlinda mlango wa timu ya Stoke City Asmir Begovic,ambaye jina lake limefanikiwa kuandikwa katika kitabu cha rekodi za dunia cha Guiness baada ya kufunga goli la mbali sana.Alifunga goli hilo kwenye mechi iliyopigwa mwezi Novemba mwaka jana kati ya Stoke City na Southampton iliyoisha kwa suluhu ya 1-1,Alifunga goli hilo akiwa umbali wa mita 91.9 toka lango la wapinzani.

                                   KWA HABARI ZAIDI>>>

"KATIKA KARNE YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA,MAJI NI ANASA NA SIO HITAJI LA MUHIMU LA BINADAMU"

Baada ya miaka 30 ya njaa iliyokithiri nchini Ethiopia,bado upatikanaji wa maji ni wa mashaka hasa ukizingatia umuhimu weneyewe wa maji kwa binadamu kama usemi maarufu usemao maarufu ''MAJI NI UHAI''.Ikiwa asilimia 52 ya watu wote inapata huduma bora za maji lakini,asilimia 10 pekee ndio waliounganishiwa bomba hadi majumbani mwao.Katika maeneo ya vijijini ni asilimia 1 tu  iliyounganishwa na huduma hii muhimu katika maisha ya binadamu..


KWA HABARI ZAIDI>>>

Hii ina maana kubwa sana.Kwa nchi ambayo uchumi wake unategemea Kilimo,upungufu wa maji hauathiri Uchumi pekee bali  unaathiri maisha ya kila siku ya wakazi hawa ambao kujikimu kwao kunategemea mavuno ya kila msimu.Mara nyingi nchi maskini kama ya Ethiopia,yenye wakazi wengi,inakumbwa sana na janga la kukosekana kwa huduma ya maji.


Kuna mambo mengi yanayochangia ukosefu wa maji safi na salama,kuanzia uharibifu wa Mazingira unaosababishwa na ukataji ovyo wa miti,majanga ya kiasili kama Mafuriko na mabadiliko ya tabia nchi....!!!


Thursday 4 September 2014

"ABIRIA KADHAA WAHOFIWA KUFA BAADA YA BASI KUSOMBWA NA MAFURIKO"


Takribani abiria 70 wanahofiwa kufa baada ya basi walilokuwa wakisafiria kusombwa na mafuriko katika jimbo la Kashmir,inaripotiwa.Ajali hiyo iliyotokea Alhamisi Kusini mwa Wilaya ya Rajouri katika ukanda wa Himalaya ambapo imekumbwa na mafuriko makali tangu miaka 22.

Wednesday 3 September 2014

"HII INAUMA,JAMAA WAKUTWA HAWANA HATIA BAADA YA KUFUNGWA JELA KWA MIAKA 30"


Vipimo vya vinasaba vilionesha ndugu hao wawili,ambao wana matatizo ya akili pia walikua ni vijana wadogo chini ya umri wa miaka 20,walioingia hatiani kimakosa tangu 1983.Wawili hao waliachiwa huru baada ya kutumikia kifungo cha miaka 30 ikiwa ni sawa na Miongo mitatu,jela kwa kesi ya Ubakaji na Mauaji ya binti wa miaka 11 baada ya ushahidi kuwekwa wazi kupitia vipimo vya vinasaba.Machungu na manung'uniko yao hayatakwisha kamwe.